< Zaburi 16 >

1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
Michtham de David. GUÁRDAME, oh Dios, porque en ti he confiado.
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
Dijiste, [oh alma mía], á Jehová: Tú eres el Señor: mi bien á ti no [aprovecha];
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
[Sino] á los santos que están en la tierra, y á los íntegros: toda mi afición en ellos.
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
Multiplicaránse los dolores de aquellos que sirven diligentes á otro [dios]: no ofreceré yo sus libaciones de sangre, ni en mis labios tomaré sus nombres.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
Jehová es la porción de mi parte y de mi copa; tú sustentarás mi suerte.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
Las cuerdas me cayeron en lugares deleitosos, y es hermosa la heredad que me ha tocado.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
Bendeciré á Jehová que me aconseja: aun en las noches me enseñan mis riñones.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
A Jehová he puesto siempre delante de mí: porque está á mi diestra no seré conmovido.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Alegróse por tanto mi corazón, y se gozó mi gloria: también mi carne reposará segura.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol h7585)
Porque no dejarás mi alma en el sepulcro; ni permitirás que tu santo vea corrupción. (Sheol h7585)
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
Me mostrarás la senda de la vida: hartura de alegrías hay con tu rostro; deleites en tu diestra para siempre.

< Zaburi 16 >