< Zaburi 16 >

1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
מכתם לדוד שמרני אל כי חסיתי בך׃
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
אמרת ליהוה אדני אתה טובתי בל עליך׃
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
לקדושים אשר בארץ המה ואדירי כל חפצי בם׃
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
ירבו עצבותם אחר מהרו בל אסיך נסכיהם מדם ובל אשא את שמותם על שפתי׃
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
יהוה מנת חלקי וכוסי אתה תומיך גורלי׃
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
חבלים נפלו לי בנעמים אף נחלת שפרה עלי׃
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
אברך את יהוה אשר יעצני אף לילות יסרוני כליותי׃
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
שויתי יהוה לנגדי תמיד כי מימיני בל אמוט׃
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
לכן שמח לבי ויגל כבודי אף בשרי ישכן לבטח׃
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol h7585)
כי לא תעזב נפשי לשאול לא תתן חסידך לראות שחת׃ (Sheol h7585)
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
תודיעני ארח חיים שבע שמחות את פניך נעמות בימינך נצח׃

< Zaburi 16 >