< Zaburi 16 >

1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
מכתם לדוד שמרני אל כי-חסיתי בך
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
אמרת ליהוה אדני אתה טובתי בל-עליך
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
לקדושים אשר-בארץ המה ואדירי כל-חפצי-בם
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
ירבו עצבותם אחר מהרו בל-אסיך נסכיהם מדם ובל-אשא את-שמותם על-שפתי
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
יהוה מנת-חלקי וכוסי-- אתה תומיך גורלי
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
חבלים נפלו-לי בנעמים אף-נחלת שפרה עלי
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
אברך--את-יהוה אשר יעצני אף-לילות יסרוני כליותי
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
שויתי יהוה לנגדי תמיד כי מימיני בל-אמוט
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
לכן שמח לבי--ויגל כבודי אף-בשרי ישכן לבטח
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol h7585)
כי לא-תעזב נפשי לשאול לא-תתן חסידך לראות שחת (Sheol h7585)
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
תודיעני ארח חיים שבע שמחות את-פניך נעמות בימינך נצח

< Zaburi 16 >