< Zaburi 16 >
1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
Verko de David. Gardu min, ho Dio, ĉar mi rifuĝas ĉe Vi.
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
Mi diris al la Eternulo: Vi estas mia Sinjoro; Mi ne havas alian bonon krom Vi.
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
Al la sanktuloj, kiuj estas sur la tero, Kaj al la majestuloj iras mia tuta deziro.
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
Multiĝos la malĝojoj de tiuj, kiuj sekvis alian; Mi ne verŝos iliajn sangajn verŝoferojn Kaj ne metos iliajn nomojn en mian buŝon.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
La Eternulo estas mia sorta parto kaj kaliko; Vi subtenas mian sorton.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
Loto agrabla trafis min, Ĉarma estas mia heredo.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
Mi gloras la Eternulon, kiu konsilas min; Eĉ en la nokto instruas min mia internaĵo.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
Ĉiam mi vidas la Eternulon antaŭ mi; Ĉar Li estas ĉe mia dekstra mano, mi ne falos.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Tial ĝojas mia koro, raviĝas mia animo; Eĉ mia karno ripozas senzorge.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol )
Ĉar Vi ne lasos mian animon al Ŝeol; Vi ne permesos, ke Via sanktulo forputru. (Sheol )
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
Vi konigos al mi la vojon de la vivo; Multe da ĝojoj estas antaŭ Vi, Ĉarmoj estas en Via dekstra mano eterne.