< Zaburi 16 >
1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
Michtam of David. Preserve me, O God: for in thee do I put my trust.
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
O my soul, thou hast said to the LORD, Thou art my Lord: my goodness extendeth not to thee;
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
But to the saints that are in the earth, and to the excellent, in whom is all my delight.
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
Their sorrows shall be multiplied that hasten after another god: their drink offerings of blood will I not offer, nor take their names into my lips.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
The LORD is the portion of my inheritance and of my cup: thou maintainest my lot.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
The lines have fallen to me in pleasant places; yea, I have a goodly heritage.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
I will bless the LORD, who hath given me counsel: my reins also instruct me in the night season.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
I have set the LORD always before me: because he is at my right hand, I shall not be moved.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Therefore my heart is glad, and my glory rejoiceth: my flesh also shall rest in hope.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol )
For thou wilt not leave my soul in hell; neither wilt thou permit thy Holy One to see corruption. (Sheol )
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
Thou wilt show me the path of life: in thy presence is fulness of joy; at thy right hand are pleasures for evermore.