< Zaburi 16 >
1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
Michtam of David. Preserve me, O God: for in thee do I put my trust.
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
I have said unto the LORD, Thou art my Lord: I have no good beyond thee.
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
As for the saints that are in the earth, they are the excellent in whom is all my delight.
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
Their sorrows shall be multiplied that exchange [the LORD] for another [god]: their drink offerings of blood will I not offer, nor take their names upon my lips.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
The LORD is the portion of mine inheritance and of my cup: thou maintainest my lot.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
The lines are fallen unto me in pleasant places; yea, I have a goodly heritage.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
I will bless the LORD, who hath given me counsel: yea, my reins instruct me in the night seasons.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
I have set the LORD always before me: because he is at my right hand, I shall not be moved.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Therefore my heart is glad, and my glory rejoiceth: my flesh also shall dwell in safety.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol )
For thou wilt not leave my soul to Sheol; neither wilt thou suffer thine holy one to see corruption. (Sheol )
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
Thou wilt shew me the path of life: in thy presence is fulness of joy; in thy right hand there are pleasures for evermore.