< Zaburi 16 >
1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
“A psalm off David.” Preserve me, O God! for to thee do I look for help.
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
I have said to Jehovah, Thou art my Lord; I have no happiness beyond thee!
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
The holy that are in the land, and the excellent, —in them is all my delight.
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
They who hasten after other gods shall have multiplied sorrows; Their drink-offerings of blood I will not offer, Nor will I take their names upon my lips.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
Jehovah is my portion and my cup; Thou wilt maintain my lot!
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
My portion hath fallen to me in pleasant places; Yea, I have a goodly inheritance.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
I will bless the LORD, who careth for me; Yea, in the night my heart admonisheth me.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
I set the LORD before me at all times; Since he is at my right hand, I shall not fall.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Therefore my heart is glad, and my spirit rejoiceth; Yea, my flesh dwelleth in security.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol )
For thou wilt not give me up to the underworld; Nor wilt thou suffer thy holy one to see the pit. (Sheol )
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
Thou wilt show me the path of life; In thy presence is fulness of joy; At thy right hand are pleasures for evermore.