< Zaburi 16 >

1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
Michtam of Dauid. Preserue mee, O God: for in thee doe I trust.
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
O my soule, thou hast sayd vnto the Lord, Thou art my Lord: my weldoing extendeth not to thee,
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
But to the Saints that are in the earth, and to the excellent: all my delite is in them.
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
The sorowes of them, that offer to an other god, shall be multiplied: their offerings of blood will I not offer, neither make mention of their names with my lips.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
The Lord is the portion of mine inheritance and of my cup: thou shalt mainteine my lot.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
The lines are fallen vnto me in pleasant places: yea, I haue a faire heritage.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
I wil prayse the Lord, who hath giuen me counsell: my reines also teach me in the nightes.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
I haue set the Lord alwayes before me: for hee is at my right hand: therefore I shall not slide.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Wherefore mine heart is glad and my tongue reioyceth: my flesh also doeth rest in hope.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol h7585)
For thou wilt not leaue my soule in the graue: neither wilt thou suffer thine holy one to see corruption. (Sheol h7585)
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
Thou wilt shew me the path of life: in thy presence is the fulnesse of ioy: and at thy right hand there are pleasures for euermore.

< Zaburi 16 >