< Zaburi 16 >
1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
A psalm (miktam) of David. Take care of me, Lord, for I come to you for protection.
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
I tell the Lord, “Apart from you Lord, I don't have anything that's good.”
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
As for the holy people in the land, they are the ones who are truly great. I appreciate them.
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
Those who run after other gods will face a lot of trouble. I will not participate in their offerings of blood, I will not even speak the names of their gods.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
Lord, you alone are all I have; you give me what I need; you safeguard my future.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
The land divisions have worked out in my favor—my property is wonderful!
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
I will bless the Lord who gives me good advice; even at night my conscience tells me what is right.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
I have always kept the Lord in front of me. I will not be shaken, for he is right beside me.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
That's why I'm so happy! That's why I am full of joy! That's why my body lives in hope!
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol )
For you will not abandon me in the grave, nor will you allow your Holy One to experience decay. (Sheol )
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
You have shown me the path of life, filling me with joy with your presence and the delight of living with you forever.