< Zaburi 16 >
1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
A Miktam of David. Preserve me, O God, for in You I take refuge.
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
I said to the LORD, “You are my Lord; apart from You I have no good thing.”
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
As for the saints in the land, they are the excellence in whom all my delight resides.
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
Sorrows will multiply to those who chase other gods. I will not pour out their libations of blood, or speak their names with my lips.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
The LORD is my chosen portion and my cup; You have made my lot secure.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
The lines of my boundary have fallen in pleasant places; surely my inheritance is delightful.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
I will bless the LORD who counsels me; even at night my conscience instructs me.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
I have set the LORD always before me. Because He is at my right hand, I will not be shaken.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Therefore my heart is glad and my tongue rejoices; my body also will dwell securely.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol )
For You will not abandon my soul to Sheol, nor will You let Your Holy One see decay. (Sheol )
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
You have made known to me the path of life; You will fill me with joy in Your presence, with eternal pleasures at Your right hand.