< Zaburi 16 >

1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
A Miktam of David. Preserve me, O God, for in You I take refuge.
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
I said to the LORD, “You are my Lord; apart from You I have no good thing.”
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
As for the saints in the land, they are the excellence in whom all my delight resides.
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
Sorrows will multiply to those who chase other gods. I will not pour out their libations of blood, or speak their names with my lips.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
The LORD is my chosen portion and my cup; You have made my lot secure.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
The lines of my boundary have fallen in pleasant places; surely my inheritance is delightful.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
I will bless the LORD who counsels me; even at night my conscience instructs me.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
I have set the LORD always before me. Because He is at my right hand, I will not be shaken.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Therefore my heart is glad and my tongue rejoices; my body also will dwell securely.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol h7585)
For You will not abandon my soul to Sheol, nor will You let Your Holy One see decay. (Sheol h7585)
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
You have made known to me the path of life; You will fill me with joy in Your presence, with eternal pleasures at Your right hand.

< Zaburi 16 >