< Zaburi 16 >

1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
Michtam of David. Preserve me, O God; for in thee do I take refuge.
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
[O my soul], thou hast said unto Jehovah, Thou art my Lord: I have no good beyond thee.
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
As for the saints that are in the earth, They are the excellent in whom is all my delight.
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
Their sorrows shall be multiplied that give gifts for another [god]: Their drink-offerings of blood will I not offer, Nor take their names upon my lips.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
Jehovah is the portion of mine inheritance and of my cup: Thou maintainest my lot.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
The lines are fallen unto me in pleasant places; Yea, I have a goodly heritage.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
I will bless Jehovah, who hath given me counsel; Yea, my heart instructeth me in the night seasons.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
I have set Jehovah always before me: Because he is at my right hand, I shall not be moved.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Therefore my heart is glad, and my glory rejoiceth: My flesh also shall dwell in safety.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol h7585)
For thou wilt not leave my soul to Sheol; Neither wilt thou suffer thy holy one to see corruption. (Sheol h7585)
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
Thou wilt show me the path of life: In thy presence is fulness of joy; In thy right hand there are pleasures for evermore.

< Zaburi 16 >