< Zaburi 16 >
1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
(En miktam af David.) Vogt mig, Gud, thi jeg lider på dig!
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
Jeg siger til HERREN: "Du er min Herre; jeg har ikke andet Gode end dig.
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
De hellige, som er i Landet, de er de herlige, hvem al min Hu står til."
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
Mange Kvaler rammer dem, som vælger en anden Gud; deres Blodofre vil jeg ikke udgyde, ej tage deres Navn i min Mund.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
HERREN er min tilmålte Del og mit Bæger. Du holder min Arvelod i Hævd.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
Snorene faldt mig på liflige Steder, ja, en dejlig Arvelod tilfaldt mig.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
Jeg vil prise HERREN, der gav mig Råd, mine Nyrer maner mig, selv om Natten.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
Jeg har altid HERREN for Øje, han er ved min højre, jeg rokkes ikke.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Derfor glædes mit Hjerte, min Ære jubler, endogså mit Kød skal bo i Tryghed.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol )
Thi Dødsriget giver du ikke min Sjæl, lader ikke din hellige skue Graven. (Sheol )
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
Du lærer mig Livets Vej; man mættes af Glæde for dit Åsyn, Livsalighed er i din højre for evigt.