< Zaburi 16 >

1 Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.
(En miktam af David.) Vogt mig, Gud, thi jeg lider på dig!
2 Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”
Jeg siger til HERREN: "Du er min Herre; jeg har ikke andet Gode end dig.
3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.
De hellige, som er i Landet, de er de herlige, hvem al min Hu står til."
4 Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.
Mange Kvaler rammer dem, som vælger en anden Gud; deres Blodofre vil jeg ikke udgyde, ej tage deres Navn i min Mund.
5 Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
HERREN er min tilmålte Del og mit Bæger. Du holder min Arvelod i Hævd.
6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.
Snorene faldt mig på liflige Steder, ja, en dejlig Arvelod tilfaldt mig.
7 Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
Jeg vil prise HERREN, der gav mig Råd, mine Nyrer maner mig, selv om Natten.
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
Jeg har altid HERREN for Øje, han er ved min højre, jeg rokkes ikke.
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,
Derfor glædes mit Hjerte, min Ære jubler, endogså mit Kød skal bo i Tryghed.
10 kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol h7585)
Thi Dødsriget giver du ikke min Sjæl, lader ikke din hellige skue Graven. (Sheol h7585)
11 Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.
Du lærer mig Livets Vej; man mættes af Glæde for dit Åsyn, Livsalighed er i din højre for evigt.

< Zaburi 16 >