< Zaburi 15 >

1 Zaburi ya Daudi. Bwana, ni nani awezaye kukaa katika Hekalu lako? Nani awezaye kuishi katika mlima wako mtakatifu?
מזמור לדוד יהוה מי יגור באהלך מי ישכן בהר קדשך׃
2 Ni yule aendaye pasipo mawaa, atendaye yaliyo haki, asemaye kweli toka moyoni mwake,
הולך תמים ופעל צדק ודבר אמת בלבבו׃
3 na hana masingizio ulimini mwake, asiyemtenda jirani yake vibaya, na asiyemsingizia mwenzake,
לא רגל על לשנו לא עשה לרעהו רעה וחרפה לא נשא על קרבו׃
4 ambaye humdharau mtu mbaya, lakini huwaheshimu wale wamwogopao Bwana, yule atunzaye kiapo chake hata kama anaumia.
נבזה בעיניו נמאס ואת יראי יהוה יכבד נשבע להרע ולא ימר׃
5 Yeye akopeshaye fedha yake bila riba, na hapokei rushwa dhidi ya mtu asiye na hatia. Mtu afanyaye haya kamwe hatatikisika.
כספו לא נתן בנשך ושחד על נקי לא לקח עשה אלה לא ימוט לעולם׃

< Zaburi 15 >