< Zaburi 149 >

1 Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
Alelu-JAH. Cantad al SEÑOR canción nueva; su alabanza sea en la congregación de los misericordiosos.
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
Alégrese Israel con su Hacedor; los hijos de Sion se gocen con su Rey.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Alaben su Nombre con baile; con adufe y arpa canten a él.
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
Porque el SEÑOR toma contentamiento con su pueblo; hermoseará a los humildes con salud.
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Se gozarán los misericordiosos con gloria; cantarán sobre sus camas.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
Ensalzamientos de Dios modularán en sus gargantas; y espadas de dos filos habrá en sus manos;
7 ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
para hacer venganza de los gentiles, castigos en los pueblos;
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
para aprisionar sus reyes en grillos, y sus nobles en cadenas de hierro;
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
para ejecutar en ellos el juicio escrito; gloria será esto para todos sus misericordiosos. Alelu-JAH.

< Zaburi 149 >