< Zaburi 149 >

1 Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
Aleluya. CANTAD á Jehová canción nueva: su alabanza [sea] en la congregación de los santos.
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
Alégrese Israel en su Hacedor: los hijos de Sión se gocen en su Rey.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Alaben su nombre con corro: con adufe y arpa á él canten.
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
Porque Jehová toma contentamiento con su pueblo: hermoseará á los humildes con salud.
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Gozarse han los píos con gloria: cantarán sobre sus camas.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
Ensalzamientos de Dios [modularán] en sus gargantas, y espadas de dos filos [habrá] en sus manos;
7 ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
Para hacer venganza de las gentes, y castigo en los pueblos;
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
Para aprisionar sus reyes en grillos, y sus nobles con cadenas de hierro;
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
Para ejecutar en ellos el juicio escrito: gloria [será] esta para todos sus santos. Aleluya.

< Zaburi 149 >