< Zaburi 149 >

1 Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
Cantád a Jehová canción nueva: su alabanza sea en la congregación de los misericordiosos.
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
Alégrese Israel con su hacedor: los hijos de Sión se regocijen con su Rey.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Alaben su nombre con corro: con adufe y arpa canten a él.
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
Porque Jehová toma contentamiento con su pueblo: hermoseará a los humildes con salud.
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Regocijarse han los piadosos con gloria: cantarán sobre sus camas.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
Ensalzamientos de Dios estarán en sus gargantas; y espadas de dos filos en sus manos:
7 ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
Para hacer venganza de los Gentiles: castigos en los pueblos.
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
Para aprisionar a sus reyes en grillos; y a sus nobles en cadenas de hierro.
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
Para hacer en ellos el juicio escrito: esta será la gloria de todos sus piadosos. Alelu- Jah.

< Zaburi 149 >