< Zaburi 149 >

1 Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
¡Alabado sea Yahvé! Canta a Yahvé una nueva canción, su alabanza en la asamblea de los santos.
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
Que Israel se regocije en el que los hizo. Que los hijos de Sión se alegren en su Rey.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
¡Que alaben su nombre en la danza! Que le canten alabanzas con pandereta y arpa.
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
Porque Yahvé se complace en su pueblo. Corona a los humildes con la salvación.
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Que los santos se regocijen en el honor. Que canten de alegría en sus camas.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
Que las altas alabanzas de Dios estén en sus bocas, y una espada de dos filos en la mano,
7 ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
para ejecutar la venganza sobre las naciones, y castigos a los pueblos;
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
para atar a sus reyes con cadenas, y sus nobles con grilletes de hierro;
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
para ejecutar en ellos la sentencia escrita. Todos sus santos tienen este honor. ¡Alabado sea Yah!

< Zaburi 149 >