< Zaburi 149 >

1 Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
Louvai ao Senhor. cantai ao Senhor um cântico novo, e o seu louvor na congregação dos santos.
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
Alegre-se Israel naquele que o fez, gozem-se os filhos de Sião no seu rei.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Louvem o seu nome com flauta; cantem-lhe o seu louvor com adufe e harpa.
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
Porque o Senhor se agrada do seu povo; ornará os mansos com a salvação.
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Exultem os santos na glória, alegrem-se nas suas camas.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
Estejam na sua garganta os altos louvores de Deus, e espada de dois fios nas suas mãos,
7 ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
Para tomarem vingança das nações, e darem repreensões aos povos;
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
Para aprisionarem os seus reis com cadeias, e os seus nobres com grilhões de ferro;
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
Para fazerem neles o juízo escrito; esta será a glória de todos os santos. louvai ao Senhor.

< Zaburi 149 >