< Zaburi 149 >
1 Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
Alleluja. [Cantate Domino canticum novum; laus ejus in ecclesia sanctorum.
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
Lætetur Israël in eo qui fecit eum, et filii Sion exsultent in rege suo.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Laudent nomen ejus in choro; in tympano et psalterio psallant ei.
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
Quia beneplacitum est Domino in populo suo, et exaltabit mansuetos in salutem.
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Exsultabunt sancti in gloria; lætabuntur in cubilibus suis.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
Exaltationes Dei in gutture eorum, et gladii ancipites in manibus eorum:
7 ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
ad faciendam vindictam in nationibus, increpationes in populis;
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
ad alligandos reges eorum in compedibus, et nobiles eorum in manicis ferreis;
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
ut faciant in eis judicium conscriptum: gloria hæc est omnibus sanctis ejus. Alleluja.]