< Zaburi 149 >
1 Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
Alleluia. Cantate all’Eterno un nuovo cantico, cantate la sua lode nell’assemblea dei fedeli.
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
Si rallegri Israele in colui che lo ha fatto, esultino i figliuoli di Sion nel loro re.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Lodino il suo nome con danze, gli salmeggino col timpano e la cetra,
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
perché l’Eterno prende piacere nel suo popolo, egli adorna di salvezza gli umili.
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Esultino i fedeli adorni di gloria, cantino di gioia sui loro letti.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
Abbiano in bocca le alte lodi di Dio, una spada a due tagli in mano
7 ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
per far vendetta delle nazioni e infligger castighi ai popoli;
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
per legare i loro re con catene e i loro nobili con ceppi di ferro,
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
per eseguir su loro il giudizio scritto. Questo è l’onore che hanno tutti i suoi fedeli. Alleluia.