< Zaburi 149 >

1 Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
הללו יה שירו ליהוה שיר חדש תהלתו בקהל חסידים׃
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
ישמח ישראל בעשיו בני ציון יגילו במלכם׃
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
יהללו שמו במחול בתף וכנור יזמרו לו׃
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
כי רוצה יהוה בעמו יפאר ענוים בישועה׃
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
יעלזו חסידים בכבוד ירננו על משכבותם׃
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
רוממות אל בגרונם וחרב פיפיות בידם׃
7 ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
לעשות נקמה בגוים תוכחת בל אמים׃
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
לאסר מלכיהם בזקים ונכבדיהם בכבלי ברזל׃
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
לעשות בהם משפט כתוב הדר הוא לכל חסידיו הללו יה׃

< Zaburi 149 >