< Zaburi 149 >

1 Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
Hallelujah! Sing to the LORD a new song— His praise in the assembly of the godly.
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
Let Israel rejoice in their Maker; let the children of Zion rejoice in their King.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Let them praise His name with dancing, and make music to Him with tambourine and harp.
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
For the LORD takes pleasure in His people; He adorns the afflicted with salvation.
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Let the saints exult in glory; let them shout for joy upon their beds.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
May the high praises of God be in their mouths, and a double-edged sword in their hands,
7 ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
to inflict vengeance on the nations and punishment on the peoples,
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
to bind their kings with chains and their nobles with shackles of iron,
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
to execute the judgment written against them. This honor is for all His saints. Hallelujah!

< Zaburi 149 >