< Zaburi 148 >

1 Msifuni Bwana. Msifuni Bwana kutoka mbinguni, msifuni juu vileleni.
Yabi Ubangiji. Yabi Ubangiji daga sammai, yabe shi a bisa sammai.
2 Msifuni, enyi malaika wake wote, msifuni yeye, enyi jeshi lake lote la mbinguni.
Yabe shi, dukanku mala’ikunsa, yabe shi, dukanku rundunarsa na sama.
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi, msifuni yeye, enyi nyota zote zingʼaazo.
Yabe shi, rana da wata, yabe shi, dukanku taurari masu haskakawa.
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu sana, na ninyi maji juu ya anga.
Yabe shi, ku bisa sammai da kuma ku ruwan bisa sarari.
5 Vilisifu jina la Bwana kwa maana aliamuru navyo vikaumbwa.
Bari su yabi sunan Ubangiji, gama ya umarta aka kuwa halicce su.
6 Aliviweka mahali pake milele na milele, alitoa amri ambayo haibadiliki milele.
Ya sa su a wurarensu har abada abadin; ya ba da umarnin da ba zai taɓa shuɗe ba.
7 Mtukuzeni Bwana kutoka duniani, ninyi viumbe vikubwa vya baharini na vilindi vyote vya bahari,
Yabi Ubangiji daga duniya, ku manyan halittun teku da kuma dukan zurfafan teku,
8 umeme wa radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu, pepo za dhoruba zinazofanya amri zake,
walƙiya da ƙanƙara, dusar ƙanƙara da gizagizai, hadirin iskar da suke biyayya da umarnansa,
9 ninyi milima na vilima vyote, miti ya matunda na mierezi yote,
ku duwatsu da dukan tuddai, itatuwa masu’ya’ya da dukan al’ul,
10 wanyama wa mwituni na mifugo yote, viumbe vidogo na ndege warukao,
namun jeji da dukan dabbobin gida, ƙanana halittu da tsuntsaye masu firiya,
11 wafalme wa dunia na mataifa yote, ninyi wakuu na watawala wote wa dunia,
sarakunan duniya da dukan al’ummai, ku sarakuna da dukan masu mulkin duniya,
12 wanaume vijana na wanawali, wazee na watoto.
samari da’yan mata, tsofaffi da yara.
13 Wote na walisifu jina la Bwana, kwa maana jina lake pekee limetukuka, utukufu wake uko juu ya nchi na mbingu.
Bari su yabi sunan Ubangiji, gama sunansa ne kaɗai mafi ɗaukaka; darajarsa ta fi ƙarfin duniya da sammai.
14 Amewainulia watu wake pembe, sifa ya watakatifu wake wote, ya Israeli, watu walio karibu na moyo wake. Msifuni Bwana.
Ya tayar wa mutanensa ƙaho, yabon dukan tsarkakansa, na Isra’ila, mutanen da suke kurkusa da zuciyarsa. Yabi Ubangiji.

< Zaburi 148 >