< Zaburi 148 >
1 Msifuni Bwana. Msifuni Bwana kutoka mbinguni, msifuni juu vileleni.
你們要讚美耶和華! 從天上讚美耶和華, 在高處讚美他!
2 Msifuni, enyi malaika wake wote, msifuni yeye, enyi jeshi lake lote la mbinguni.
他的眾使者都要讚美他! 他的諸軍都要讚美他!
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi, msifuni yeye, enyi nyota zote zingʼaazo.
日頭月亮,你們要讚美他! 放光的星宿,你們都要讚美他!
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu sana, na ninyi maji juu ya anga.
天上的天和天上的水, 你們都要讚美他!
5 Vilisifu jina la Bwana kwa maana aliamuru navyo vikaumbwa.
願這些都讚美耶和華的名! 因他一吩咐便都造成。
6 Aliviweka mahali pake milele na milele, alitoa amri ambayo haibadiliki milele.
他將這些立定,直到永永遠遠; 他定了命,不能廢去。
7 Mtukuzeni Bwana kutoka duniani, ninyi viumbe vikubwa vya baharini na vilindi vyote vya bahari,
所有在地上的, 大魚和一切深洋,
8 umeme wa radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu, pepo za dhoruba zinazofanya amri zake,
火與冰雹,雪和霧氣, 成就他命的狂風,
9 ninyi milima na vilima vyote, miti ya matunda na mierezi yote,
大山和小山, 結果的樹木和一切香柏樹,
10 wanyama wa mwituni na mifugo yote, viumbe vidogo na ndege warukao,
野獸和一切牲畜, 昆蟲和飛鳥,
11 wafalme wa dunia na mataifa yote, ninyi wakuu na watawala wote wa dunia,
世上的君王和萬民, 首領和世上一切審判官,
12 wanaume vijana na wanawali, wazee na watoto.
少年人和處女, 老年人和孩童, 都當讚美耶和華!
13 Wote na walisifu jina la Bwana, kwa maana jina lake pekee limetukuka, utukufu wake uko juu ya nchi na mbingu.
願這些都讚美耶和華的名! 因為獨有他的名被尊崇; 他的榮耀在天地之上。
14 Amewainulia watu wake pembe, sifa ya watakatifu wake wote, ya Israeli, watu walio karibu na moyo wake. Msifuni Bwana.
他將他百姓的角高舉, 因此他一切聖民以色列人, 就是與他相近的百姓,都讚美他! 你們要讚美耶和華!