< Zaburi 147 >

1 Msifuni Bwana. Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa, jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye!
ヱホバをほめたたへよ われらの神をほめうたふは善ことなり樂しきことなり 稱へまつるはよろしきに適へり
2 Bwana hujenga Yerusalemu, huwakusanya Israeli walio uhamishoni.
ヱホバはヱルサレムをきづきイスラエルのさすらへる者をあつめたまふ
3 Anawaponya waliovunjika mioyo na kuvifunga vidonda vyao.
ヱホバは心のくだけたるものを醫しその傷をつつみたまふ
4 Huzihesabu nyota na huipa kila moja jina lake.
ヱホバはもろもろの星の數をかぞへてすべてこれに名をあたへたまふ
5 Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi, ufahamu wake hauna kikomo.
われらの主はおほいなりその能力もまた大なりその智慧はきはまりなし
6 Bwana huwahifadhi wanyenyekevu lakini huwashusha waovu mpaka mavumbini.
ヱホバは柔和なるものをささへ屈きものを地にひきおとし給ふ
7 Mwimbieni Bwana kwa shukrani, mpigieni Mungu wetu kinubi.
ヱホバに感謝してうたへ琴にあはせてわれらの神をほめうたヘ
8 Yeye huzifunika anga kwa mawingu, huinyeshea ardhi mvua, na kuzifanya nyasi kuota juu ya vilima.
ヱホバは雲をもて天をおほひ地のために雨をそなへ もろもろの山に草をはえしめ
9 Huwapa chakula mifugo na pia makinda ya kunguru yanapolia.
くひものを獣にあたへ並なく小鴉にあたへたまふ
10 Furaha yake haipo katika nguvu za farasi, wala furaha yake kwenye miguu ya mwanadamu.
ヱホバは馬のちからを喜びたまはず 人の足をよみしたまはず
11 Bwana hupendezwa na wale wamchao, wale wanaoweka tumaini lao katika upendo wake usiokoma.
ヱホバはおのれを畏るるものと おのれの憐憫をのぞむものとを好したまふ
12 Mtukuze Bwana, ee Yerusalemu, msifu Mungu wako, ee Sayuni,
ヱルサレムよヱホバをほめたたへよ シオンよなんぢの神をほめたたへよ
13 kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako na huwabariki watu wako walio ndani yako.
ヱホバはなんぢの門の関木をかたうし 汝のうちなる子輩をさきはひ給ひたればなり
14 Huwapa amani mipakani mwenu na kukushibisha kwa ngano safi kabisa.
ヱホバは汝のすべての境にやはらぎをあたへ いと嘉麥をもて汝をあかしめたまふ
15 Hutuma amri yake duniani, neno lake hukimbia kasi.
ヱホバはそのいましめを地にくだしたまふ その聖言はいとずみやかにはしる
16 Anatandaza theluji kama sufu na kutawanya umande kama majivu.
ヱホバは雪をひつじの毛のごとくふらせ霜を灰のごとくにまきたまふ
17 Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe. Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?
ヱホバは氷をつちくれのごとくに擲ちたまふ たれかその寒冷にたふることをえんや
18 Hutuma neno lake na kuviyeyusha, huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.
ヱホバ聖言をくだしてこれを消し その風をふかしめたまへばもろもろの水はながる
19 Amemfunulia Yakobo neno lake, sheria zake na maagizo yake kwa Israeli.
ヱホバはそのみことばをヤコブに示し そのもろもろの律法とその審判とをイスラエルにしめしたまふ
20 Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote, hawazijui sheria zake. Msifuni Bwana.
ヱホバはいづれの國をも如此あしらひたまひしにあらず ヱホバのもろもろの審判をかれらはしらざるなり ヱホバをほめたたへよ

< Zaburi 147 >