< Zaburi 146 >
1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Aleluja! Hvali, duša moja, Gospoda.
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
Hvalil bodem Gospoda v življenji svojem; prepeval bodem Bogu svojemu, dokler bodem.
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
Ne imejte zaupanja v prvake, v sina človeškega, pri katerem ni blaginje.
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
Duh njegov izide, povrne se v zemljo svojo; isti dan minejo misli njegove.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Blagor, komur je na pomoč Bog mogočni Jakobov; katerega nada je v Gospodu, njegovem Bogu,
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
Kateri je naredil nebesa in zemljo, morje in kar je v njiju, kateri hrani zvestobo vekomaj.
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
Kateri dela pravico zatiranim, hrane daje lačnim, Gospod oprašča jetnike.
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
Gospod odpira očí slepim, Gospod vzdiguje potrte, Gospod ljubi pravične.
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
Gospod brani tujce, siroto in vdovo podpira; pot pa hudobnih razdira.
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
Vladal bode Gospod vekomaj; Bog tvoj, o Sijon, od roda do roda. Aleluja!