< Zaburi 146 >

1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Аллилуия. Аггея и Захарии. Хвали, душа моя, Господа.
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
Буду восхвалять Господа, доколе жив; буду петь Богу моему, доколе есмь.
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
Не надейтесь на князей, на сына человеческого, в котором нет спасения.
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
Выходит дух его, и он возвращается в землю свою: в тот день исчезают все помышления его.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Блажен, кому помощник Бог Иаковлев, у кого надежда на Господа Бога его,
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
сотворившего небо и землю, море и все, что в них, вечно хранящего верность,
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
творящего суд обиженным, дающего хлеб алчущим. Господь разрешает узников,
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
Господь отверзает очи слепым, Господь восставляет согбенных, Господь любит праведных.
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
Господь хранит пришельцев, поддерживает сироту и вдову, а путь нечестивых извращает.
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
Господь будет царствовать во веки, Бог твой, Сион, в род и род. Аллилуия.

< Zaburi 146 >