< Zaburi 146 >
1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
alleluia Aggei et Zacchariae
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
lauda anima mea Dominum laudabo Dominum in vita mea psallam Deo meo quamdiu fuero nolite confidere in principibus
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
in filiis hominum quibus non est salus
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
exibit spiritus eius et revertetur in terram suam in illa die peribunt omnes cogitationes eorum
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
beatus cuius Deus Iacob adiutor eius spes eius in Domino Deo ipsius
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
qui fecit caelum et terram mare et omnia quae in eis
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
qui custodit veritatem in saeculum facit iudicium iniuriam patientibus dat escam esurientibus Dominus solvit conpeditos
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
Dominus inluminat caecos Dominus erigit adlisos Dominus diligit iustos
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
Dominus custodit advenas pupillum et viduam suscipiet et viam peccatorum disperdet
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
regnabit Dominus in saecula Deus tuus Sion in generationem et generationem