< Zaburi 146 >

1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Praise ye the LORD. Praise the LORD, O my soul.
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
While I live will I praise the LORD: I will sing praises unto my God while I have any being.
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
Put not your trust in princes, nor in the son of man, in whom there is no help.
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
His breath goeth forth, he returneth to his earth; in that very day his thoughts perish.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Happy is he that hath the God of Jacob for his help, whose hope is in the LORD his God:
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
Which made heaven and earth, the sea, and all that in them is; which keepeth truth for ever:
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
Which executeth judgment for the oppressed; which giveth food to the hungry: the LORD looseth the prisoners;
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
The LORD openeth [the eyes of] the blind; the LORD raiseth up them that are bowed down; the LORD loveth the righteous;
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
The LORD preserveth the strangers; he upholdeth the fatherless and widow; but the way of the wicked he turneth upside down.
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
The LORD shall reign for ever, thy God, O Zion, unto all generations. Praise ye the LORD.

< Zaburi 146 >