< Zaburi 146 >

1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Hallelujah. Praise the LORD, O my soul.
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
I will praise the LORD while I live; I will sing praises unto my God while I have my being.
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
Put not your trust in princes, nor in the son of man, in whom there is no help.
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
His breath goeth forth, he returneth to his dust; in that very day his thoughts perish.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Happy is he whose help is the God of Jacob, whose hope is in the LORD his God,
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
Who made heaven and earth, the sea, and all that in them is; who keepeth truth for ever;
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
Who executeth justice for the oppressed; who giveth bread to the hungry. The LORD looseth the prisoners;
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
The LORD openeth the eyes of the blind; the LORD raiseth up them that are bowed down; the LORD loveth the righteous;
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
The LORD preserveth the strangers; He upholdeth the fatherless and the widow; but the way of the wicked He maketh crooked.
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
The LORD will reign for ever, Thy God, O Zion, unto all generations. Hallelujah.

< Zaburi 146 >