< Zaburi 146 >

1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Praise ye the Lord. Praise thou the Lord, O my soule.
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
I will prayse the Lord during my life: as long as I haue any being, I wil sing vnto my God.
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
Put not your trust in princes, nor in the sonne of man, for there is none helpe in him.
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
His breath departeth, and he returneth to his earth: then his thoughtes perish.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Blessed is he, that hath the God of Iaakob for his helpe, whose hope is in the Lord his God.
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
Which made heauen and earth, the sea, and all that therein is: which keepeth his fidelitie for euer:
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
Which executeth iustice for the oppressed: which giueth bread to the hungry: the Lord loseth the prisoners.
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
The Lord giueth sight to the blinde: the Lord rayseth vp the crooked: the Lord loueth the righteous.
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
The Lord keepeth the strangers: he relieueth the fatherlesse and widowe: but he ouerthroweth the way of the wicked.
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
The Lord shall reigne for euer: O Zion, thy God endureth from generation to generation. Prayse ye the Lord.

< Zaburi 146 >