< Zaburi 146 >
1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Alleluia, of Aggeus and Zacharias.
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
Praise the Lord, O my soul, in my life I will praise the Lord: I will sing to my God as long as I shall be. Put not your trust in princes:
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
In the children of men, in whom there is no salvation.
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
His spirit shall go forth, and he shall return into his earth: in that day all their thoughts shall perish.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Blessed is he who hath the God of Jacob for his helper, whose hope is in the Lord his God:
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
Who made heaven and earth, the sea, and all things that are in them.
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
Who keepeth truth for ever: who executeth judgment for them that suffer wrong: who giveth food to the hungry. The Lord looseth them that are fettered:
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
The Lord enlighteneth the blind. The Lord lifteth up them that are cast down: the Lord loveth the just.
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
The Lord keepeth the strangers, he will support the fatherless and the widow: and the ways of sinners he will destroy.
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
The Lord shall reign for ever: thy God, O Sion, unto generation and generation.