< Zaburi 146 >

1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Halleluja! Pris HERREN, min Sjæl!
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
Jeg vil prise HERREN hele mit Liv, lovsynge min Gud, saa længe jeg lever.
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
Sæt ikke eders Lid til Fyrster, til et Menneskebarn, der ikke kan hjælpe!
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
Hans Aand gaar bort, han bliver til Jord igen, hans Raad er bristet samme Dag.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Salig den, hvis Hjælp er Jakobs Gud, hvis Haab staar til HERREN hans Gud,
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
som skabte Himmel og Jord, Havet og alt, hvad de rummer, som evigt bevarer sin Trofasthed
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
og skaffer de undertrykte Ret, som giver de sultne Brød! HERREN løser de fangne,
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
HERREN aabner de blindes Øjne, HERREN rejser de bøjede, HERREN elsker de retfærdige,
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
HERREN vogter de fremmede, opholder faderløse og Enker, men gudløses Vej gør han kroget.
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
HERREN er Konge for evigt, din Gud, o Zion, fra Slægt til Slægt. Halleluja!

< Zaburi 146 >