< Zaburi 146 >
1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Aleluja! Hvali, dušo moja, Jahvu!
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
Hvalit ću Jahvu sveg života svojeg. Dok me bude, Bogu svom ću pjevati.
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
Ne uzdajte se u knezove, u čovjeka od kog nema spasenja!
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
Iziđe li duh iz njega, u zemlju svoju on se vraća i propadaju sve misli njegove.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Blago onom kome je pomoćnik Bog Jakovljev, kome je ufanje u Jahvi, Bogu njegovu,
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
koji stvori nebo i zemlju, more i sve što je u njima; koji ostaje vjeran dovijeka,
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
potlačenima vraća pravicu, a gladnima kruh daje. Jahve oslobađa sužnje,
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
Jahve slijepcima oči otvara. Jahve uspravlja prignute, Jahve ljubi pravedne.
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
Jahve štiti tuđince, sirote i udovice podupire, a grešnicima mrsi putove.
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
Jahve će kraljevati dovijeka, tvoj Bog, Sione, od koljena do koljena. Aleluja!