< Zaburi 145 >

1 Wimbo wa Sifa. Wa Daudi. Nitakutukuza wewe, Mungu wangu Mfalme, nitalisifu jina lako milele na milele.
ダビデのさんびの歌 わが神、王よ、わたしはあなたをあがめ、世々かぎりなくみ名をほめまつります。
2 Kila siku nitakusifu na kulitukuza jina lako milele na milele.
わたしは日ごとにあなたをほめ、世々かぎりなくみ名をほめたたえます。
3 Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, ukuu wake haupimiki.
主は大いなる神で、大いにほめたたえらるべきです。その大いなることは測り知ることができません。
4 Kizazi kimoja kitasifia kazi zako kwa kizazi kingine, watasimulia matendo yako makuu.
この代はかの代にむかってあなたのみわざをほめたたえ、あなたの大能のはたらきを宣べ伝えるでしょう。
5 Watasema juu ya utukufu wa fahari ya ukuu wako, nami nitatafakari juu ya kazi zako za ajabu.
わたしはあなたの威厳の光栄ある輝きと、あなたのくすしきみわざとを深く思います。
6 Watasimulia uwezo wa kazi zako za kutisha, nami nitatangaza matendo yako makuu.
人々はあなたの恐るべきはたらきの勢いを語り、わたしはあなたの大いなることを宣べ伝えます。
7 Wataadhimisha wema wako mwingi, na wataimba kwa shangwe juu ya haki yako.
彼らはあなたの豊かな恵みの思い出を言いあらわし、あなたの義を喜び歌うでしょう。
8 Bwana ni mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo.
主は恵みふかく、あわれみに満ち、怒ることおそく、いつくしみ豊かです。
9 Bwana ni mwema kwa wote, ana huruma kwa vyote alivyovifanya.
主はすべてのものに恵みがあり、そのあわれみはすべてのみわざの上にあります。
10 Ee Bwana, vyote ulivyovifanya vitakusifu, watakatifu wako watakutukuza.
主よ、あなたのすべてのみわざはあなたに感謝し、あなたの聖徒はあなたをほめまつるでしょう。
11 Watasimulia utukufu wa ufalme wako na kusema juu ya ukuu wako,
彼らはみ国の栄光を語り、あなたのみ力を宣べ、
12 ili watu wote wajue matendo yako makuu na utukufu wa fahari ya ufalme wako.
あなたの大能のはたらきと、み国の光栄ある輝きとを人の子に知らせるでしょう。
13 Ufalme wako ni ufalme wa milele, mamlaka yako hudumu vizazi vyote. Bwana ni mwaminifu kwa ahadi zake zote na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
あなたの国はとこしえの国です。あなたのまつりごとはよろずよに絶えることはありません。
14 Bwana huwategemeza wote waangukao, na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao.
主はすべて倒れんとする者をささえ、すべてかがむ者を立たせられます。
15 Macho yao wote yanakutazama wewe, nawe huwapa chakula chao wakati wake.
よろずのものの目はあなたを待ち望んでいます。あなたは時にしたがって彼らに食物を与えられます。
16 Waufumbua mkono wako, watosheleza haja ya kila kitu kilicho hai.
あなたはみ手を開いて、すべての生けるものの願いを飽かせられます。
17 Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
主はそのすべての道に正しく、そのすべてのみわざに恵みふかく、
18 Bwana yu karibu na wote wamwitao, karibu na wote wamwitao kwa uaminifu.
すべて主を呼ぶ者、誠をもって主を呼ぶ者に主は近いのです。
19 Huwatimizia wamchao matakwa yao, husikia kilio chao na kuwaokoa.
主はおのれを恐れる者の願いを満たし、またその叫びを聞いてこれを救われます。
20 Bwana huwalinda wote wampendao, bali waovu wote atawaangamiza.
主はおのれを愛する者をすべて守られるが、悪しき者をことごとく滅ぼされます。
21 Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana. Kila kiumbe na kilisifu jina lake takatifu milele na milele.
わが口は主の誉を語り、すべての肉なる者は世々かぎりなくその聖なるみ名をほめまつるでしょう。

< Zaburi 145 >