< Zaburi 144 >

1 Zaburi ya Daudi. Sifa ni kwa Bwana Mwamba wangu, aifundishaye mikono yangu vita, na vidole vyangu kupigana.
לדוד ברוך יהוה צורי המלמד ידי לקרב אצבעותי למלחמה׃
2 Yeye ni Mungu wangu wa upendo na boma langu, ngome yangu na mwokozi wangu, ngao yangu ninayemkimbilia, ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
חסדי ומצודתי משגבי ומפלטי לי מגני ובו חסיתי הרודד עמי תחתי׃
3 Ee Bwana, mwanadamu ni nini hata umjali, Binadamu ni nini hata umfikirie?
יהוה מה אדם ותדעהו בן אנוש ותחשבהו׃
4 Mwanadamu ni kama pumzi, siku zake ni kama kivuli kinachopita.
אדם להבל דמה ימיו כצל עובר׃
5 Ee Bwana, pasua mbingu zako, ushuke, gusa milima ili itoe moshi.
יהוה הט שמיך ותרד גע בהרים ויעשנו׃
6 Peleka umeme uwatawanye adui, lenga mishale yako uwashinde.
ברוק ברק ותפיצם שלח חציך ותהמם׃
7 Nyoosha mkono wako kutoka juu, nikomboe na kuniokoa kutoka maji makuu, kutoka mikononi mwa wageni
שלח ידיך ממרום פצני והצילני ממים רבים מיד בני נכר׃
8 ambao vinywa vyao vimejaa uongo, na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.
אשר פיהם דבר שוא וימינם ימין שקר׃
9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya, kwa zeze yenye nyuzi kumi nitakuimbia,
אלהים שיר חדש אשירה לך בנבל עשור אזמרה לך׃
10 kwa Yule awapaye wafalme ushindi, ambaye humwokoa Daudi, mtumishi wake kutokana na upanga hatari.
הנותן תשועה למלכים הפוצה את דוד עבדו מחרב רעה׃
11 Nikomboe na uniokoe kutoka mikononi mwa wageni ambao vinywa vyao vimejaa uongo, na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.
פצני והצילני מיד בני נכר אשר פיהם דבר שוא וימינם ימין שקר׃
12 Kisha wana wetu wakati wa ujana wao watakuwa kama mimea iliyotunzwa vizuri, binti zetu watakuwa kama nguzo zilizoviringwa kurembesha jumba la kifalme.
אשר בנינו כנטעים מגדלים בנעוריהם בנותינו כזוית מחטבות תבנית היכל׃
13 Ghala zetu zitajazwa aina zote za mahitaji. Kondoo zetu watazaa kwa maelfu, kwa makumi ya maelfu katika mashamba yetu;
מזוינו מלאים מפיקים מזן אל זן צאוננו מאליפות מרבבות בחוצותינו׃
14 maksai wetu watakokota mizigo mizito. Hakutakuwa na kubomoka kuta, hakuna kuchukuliwa mateka, wala kilio cha taabu katika barabara zetu.
אלופינו מסבלים אין פרץ ואין יוצאת ואין צוחה ברחבתינו׃
15 Heri watu ambao hili ni kweli; heri wale ambao Bwana ni Mungu wao.
אשרי העם שככה לו אשרי העם שיהוה אלהיו׃

< Zaburi 144 >