< Zaburi 144 >

1 Zaburi ya Daudi. Sifa ni kwa Bwana Mwamba wangu, aifundishaye mikono yangu vita, na vidole vyangu kupigana.
לדוד ברוך יהוה צורי-- המלמד ידי לקרב אצבעותי למלחמה
2 Yeye ni Mungu wangu wa upendo na boma langu, ngome yangu na mwokozi wangu, ngao yangu ninayemkimbilia, ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
חסדי ומצודתי משגבי ומפלטי-לי מגני ובו חסיתי הרודד עמי תחתי
3 Ee Bwana, mwanadamu ni nini hata umjali, Binadamu ni nini hata umfikirie?
יהוה--מה-אדם ותדעהו בן-אנוש ותחשבהו
4 Mwanadamu ni kama pumzi, siku zake ni kama kivuli kinachopita.
אדם להבל דמה ימיו כצל עובר
5 Ee Bwana, pasua mbingu zako, ushuke, gusa milima ili itoe moshi.
יהוה הט-שמיך ותרד גע בהרים ויעשנו
6 Peleka umeme uwatawanye adui, lenga mishale yako uwashinde.
ברוק ברק ותפיצם שלח חציך ותהמם
7 Nyoosha mkono wako kutoka juu, nikomboe na kuniokoa kutoka maji makuu, kutoka mikononi mwa wageni
שלח ידיך ממרום פצני והצילני ממים רבים מיד בני נכר
8 ambao vinywa vyao vimejaa uongo, na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.
אשר פיהם דבר-שוא וימינם ימין שקר
9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya, kwa zeze yenye nyuzi kumi nitakuimbia,
אלהים--שיר חדש אשירה לך בנבל עשור אזמרה-לך
10 kwa Yule awapaye wafalme ushindi, ambaye humwokoa Daudi, mtumishi wake kutokana na upanga hatari.
הנותן תשועה למלכים הפוצה את-דוד עבדו--מחרב רעה
11 Nikomboe na uniokoe kutoka mikononi mwa wageni ambao vinywa vyao vimejaa uongo, na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.
פצני והצילני מיד בני-נכר אשר פיהם דבר-שוא וימינם ימין שקר
12 Kisha wana wetu wakati wa ujana wao watakuwa kama mimea iliyotunzwa vizuri, binti zetu watakuwa kama nguzo zilizoviringwa kurembesha jumba la kifalme.
אשר בנינו כנטעים-- מגדלים בנעוריהם בנותינו כזוית-- מחטבות תבנית היכל
13 Ghala zetu zitajazwa aina zote za mahitaji. Kondoo zetu watazaa kwa maelfu, kwa makumi ya maelfu katika mashamba yetu;
מזוינו מלאים-- מפיקים מזן אל-זן צאוננו מאליפות מרבבות-- בחוצותינו
14 maksai wetu watakokota mizigo mizito. Hakutakuwa na kubomoka kuta, hakuna kuchukuliwa mateka, wala kilio cha taabu katika barabara zetu.
אלופינו מסבלים אין-פרץ ואין יוצאת ואין צוחה ברחבתינו
15 Heri watu ambao hili ni kweli; heri wale ambao Bwana ni Mungu wao.
אשרי העם שככה לו אשרי העם שיהוה אלהיו

< Zaburi 144 >