< Zaburi 144 >

1 Zaburi ya Daudi. Sifa ni kwa Bwana Mwamba wangu, aifundishaye mikono yangu vita, na vidole vyangu kupigana.
上主,我的磐石,他應該常受頌讚!他教我的手能鬥,教我的指能戰。
2 Yeye ni Mungu wangu wa upendo na boma langu, ngome yangu na mwokozi wangu, ngao yangu ninayemkimbilia, ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
他是我的力量,我的堡壘,他是我的干城,我的救主,我的盾牌及我的避難所,他使萬民都來屈服於我。
3 Ee Bwana, mwanadamu ni nini hata umjali, Binadamu ni nini hata umfikirie?
上主,世人算什麼,您竟眷顧他,人子算什麼您竟懷念他?
4 Mwanadamu ni kama pumzi, siku zake ni kama kivuli kinachopita.
世人不過像一口氣,他的歲月如影消逝。
5 Ee Bwana, pasua mbingu zako, ushuke, gusa milima ili itoe moshi.
上主,求您將天低垂,親自降凡,您一觸摸群山,群山立即冒煙。
6 Peleka umeme uwatawanye adui, lenga mishale yako uwashinde.
求您發出閃電,將敵人驅散,求您把箭射出,使他們混亂。
7 Nyoosha mkono wako kutoka juu, nikomboe na kuniokoa kutoka maji makuu, kutoka mikononi mwa wageni
求您自高處伸出您的手,救拔我,求您由洪水和外人手中,拯救我!
8 ambao vinywa vyao vimejaa uongo, na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.
他們的口舌只說虛言謊語,只是為發假誓而舉起右手。
9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya, kwa zeze yenye nyuzi kumi nitakuimbia,
天主,我要向您高唱新曲,我要彈十絃琴向您詠奏。
10 kwa Yule awapaye wafalme ushindi, ambaye humwokoa Daudi, mtumishi wake kutokana na upanga hatari.
是您賜給君王獲得了勝利,是您拯救了您的僕人達味。
11 Nikomboe na uniokoe kutoka mikononi mwa wageni ambao vinywa vyao vimejaa uongo, na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.
求您由凶險的刀劍救拔我,求您由外人的手掌拯救我!他們的口舌只說虛言謊語,只是為發假誓而舉起右手。
12 Kisha wana wetu wakati wa ujana wao watakuwa kama mimea iliyotunzwa vizuri, binti zetu watakuwa kama nguzo zilizoviringwa kurembesha jumba la kifalme.
願我們的兒子們,從幼就像茂盛的果樹,願我們的女兒們,像宮殿中雕刻的砥柱!
13 Ghala zetu zitajazwa aina zote za mahitaji. Kondoo zetu watazaa kwa maelfu, kwa makumi ya maelfu katika mashamba yetu;
願我們倉廩裡的各種食糧常滿,願我們牧場上的羊群,蕃殖億萬!
14 maksai wetu watakokota mizigo mizito. Hakutakuwa na kubomoka kuta, hakuna kuchukuliwa mateka, wala kilio cha taabu katika barabara zetu.
願我們的牲畜常滿載重量,城牆沒有缺口也沒有逃亡,我們的街市中也沒有悲傷。
15 Heri watu ambao hili ni kweli; heri wale ambao Bwana ni Mungu wao.
身逢這些福樂的百姓,真是有福,認上主為天主的人民,真是有福。

< Zaburi 144 >