< Zaburi 143 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
مزمور داوود. ای خداوند، دعای مرا بشنو و به التماس من گوش بده! تو عادل و امین هستی، پس دعایم را اجابت فرما.
2 Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
بندهٔ خود را محاکمه نکن، زیرا هیچ‌کس در نزد تو عادل و بی‌گناه نیست.
3 Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
دشمن مرا از پای درآورده و به زمین کوبیده است! روزگارم را آنچنان سیاه کرده که مرگ را در چند قدمی خود می‌بینم!
4 Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
روحیهٔ خود را به کلی باخته‌ام و از ترس نزدیک است قالب تهی کنم.
5 Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
گذشتهٔ خود را به یاد می‌آورم و به کارهایی که تو ای خدا، برای من انجام داده‌ای می‌اندیشم.
6 Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
دستهای خود را به سوی تو دراز می‌کنم. جان من همچون زمین خشک، تشنه و طالب توست!
7 Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
ای خداوند، دعای مرا هر چه زودتر اجابت فرما، زیرا نومید و مأیوسم. روی خود را از من برنگردان، مبادا بمیرم.
8 Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
هر روز صبح محبت خود را به من بنمایان، زیرا بر تو توکل دارم. راهی را که باید بپیمایم به من نشان ده، زیرا از صمیم قلب به حضور تو دعا می‌کنم.
9 Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
ای خداوند، مرا از دست دشمنانم برهان، زیرا به تو پناه آورده‌ام.
10 Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
مرا تعلیم ده تا ارادهٔ تو را بجا آورم، زیرا تو خدای من هستی. باشد که روح مهربان تو مرا به زمین هموار هدایت کند.
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
ای خداوند، به خاطر نام خود جانم را حفظ کن، به خاطر عدالت خود، مرا از این تنگی برهان.
12 Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.
بر من محبت فرما و همهٔ دشمنان و مخالفانم را نابود کن، زیرا من خدمتگزار تو هستم.

< Zaburi 143 >