< Zaburi 143 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
מזמור לדוד יהוה שמע תפלתי האזינה אל תחנוני באמנתך ענני בצדקתך׃
2 Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
ואל תבוא במשפט את עבדך כי לא יצדק לפניך כל חי׃
3 Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
כי רדף אויב נפשי דכא לארץ חיתי הושיבני במחשכים כמתי עולם׃
4 Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
ותתעטף עלי רוחי בתוכי ישתומם לבי׃
5 Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
זכרתי ימים מקדם הגיתי בכל פעלך במעשה ידיך אשוחח׃
6 Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
פרשתי ידי אליך נפשי כארץ עיפה לך סלה׃
7 Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
מהר ענני יהוה כלתה רוחי אל תסתר פניך ממני ונמשלתי עם ירדי בור׃
8 Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
השמיעני בבקר חסדך כי בך בטחתי הודיעני דרך זו אלך כי אליך נשאתי נפשי׃
9 Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
הצילני מאיבי יהוה אליך כסתי׃
10 Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
למדני לעשות רצונך כי אתה אלוהי רוחך טובה תנחני בארץ מישור׃
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
למען שמך יהוה תחיני בצדקתך תוציא מצרה נפשי׃
12 Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.
ובחסדך תצמית איבי והאבדת כל צררי נפשי כי אני עבדך׃

< Zaburi 143 >