< Zaburi 143 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
Psaume de David. Seigneur, écoute ma prière, prête l’oreille à mes supplications, dans ta fidélité réponds-moi, et dans ta bienveillance:
2 Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
n’entre pas en jugement avec ton serviteur, car nul vivant ne peut se trouver juste à tes yeux.
3 Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
C’Est que l’ennemi s’est jeté à ma poursuite, a broyé ma vie sur le sol, me plongeant dans les ténèbres, comme ceux qui, dès longtemps, appartiennent à la mort.
4 Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
Mon esprit tombe en défaillance en moi, en mon sein mon cœur est frappé de stupeur.
5 Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
J’Évoque le souvenir des jours antiques, je pense à l’ensemble de tes actes, et médite sur l’œuvre de tes mains.
6 Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
Je tends les mains vers toi; mon âme, telle une terre aride, a soif de toi. (Sélah)
7 Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
Sans retard exauce-moi, ô Seigneur, mon esprit se consume; ne me dérobe point ta face, sinon je ressemblerai à ceux qui descendent dans la tombe.
8 Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
Dès le matin, annonce-moi ta grâce, car j’ai mis confiance en toi; fais-moi connaître le chemin que je dois suivre, car vers toi j’élève mon âme.
9 Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
Délivre-moi de mes ennemis, Eternel, c’est en toi que je cherche un abri,
10 Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
Enseigne-moi à accomplir ta volonté, car c’est toi qui es mon Dieu; que ton esprit bienveillant me guide sur un sol uni!
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
En faveur de ton nom, Eternel, tu me conserveras en vie; dans ta justice, tu libéreras mon âme de la détresse.
12 Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.
Dans ta bonté, tu anéantiras mes ennemis, tu feras périr tous ceux qui me sont hostiles, car je suis ton serviteur.

< Zaburi 143 >