< Zaburi 143 >
1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
A psalm of David O Yahweh - hear prayer my give ear! to supplications my in faithfulness your answer me in righteousness your.
2 Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
And may not you go in judgment with servant your for not he is righteous before you any living [person].
3 Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
For he has pursued an enemy - self my he has crushed to the ground life my he has caused to dwell me in dark places like dead [people] of antiquity.
4 Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
And it has fainted away on me spirit my in [the] midst of me it is appalled heart my.
5 Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
I have remembered days - from antiquity I have meditated on every deed your on [the] work of hands your I meditate.
6 Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
I have spread out hands my to you throat my - like a land exhausted [is] to you (Selah)
7 Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
Hurry answer me - O Yahweh it is exhausted spirit my may not you hide face your from me and I will be equal with [those who] go down of [the] pit.
8 Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
Make hear me in the morning - covenant loyalty your for in you I have trusted make known to me [the] way which I will go for to you I lift up desire my.
9 Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
Deliver me from enemies my - O Yahweh to you I have covered.
10 Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
Teach me - to do will your for you [are] God my spirit your good may it lead me in a land of level ground.
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
For [the] sake of name your O Yahweh you will preserve alive me in righteousness your - you will bring out from trouble life my.
12 Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.
And in covenant loyalty your you will destroy enemies my and you will destroy all [the] opposers of life my for I [am] servant your.