< Zaburi 143 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
[A Psalm by David.] Hear my prayer, LORD. Listen to my petitions. In your faithfulness and righteousness, relieve me.
2 Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
Do not enter into judgment with your servant, for in your sight no man living is righteous.
3 Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
For the enemy pursues my soul. He has struck my life down to the ground. He has made me live in dark places, as those who have been long dead.
4 Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
Therefore my spirit is overwhelmed within me. My heart within me is desolate.
5 Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
I remember the days of old. I meditate on all your doings. I contemplate the work of your hands.
6 Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
I spread forth my hands to you. My soul thirsts for you, like a parched land. (Selah)
7 Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
Hurry to answer me, LORD. My spirit fails. Do not hide your face from me, so that I do not become like those who go down into the pit.
8 Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
Cause me to hear your loving kindness in the morning, for I trust in you. Cause me to know the way in which I should walk, for I lift up my soul to you.
9 Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
Deliver me, LORD, from my enemies. I run to you for refuge.
10 Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
Teach me to do your will, for you are my God. Your Spirit is good. Lead me in the land of uprightness.
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
Revive me, LORD, for your name's sake. In your righteousness, bring my soul out of trouble.
12 Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.
In your loving kindness, cut off my enemies, and destroy all those who afflict my soul, For I am your servant.

< Zaburi 143 >