< Zaburi 143 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
A PSALM OF DAVID. O YHWH, hear my prayer, Give ear to my supplications, Answer me in Your faithfulness—in Your righteousness.
2 Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
And do not enter into judgment with Your servant, For no one living is justified before You.
3 Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
For an enemy has pursued my soul, He has bruised my life to the earth, He has caused me to dwell in dark places, As the dead of old.
4 Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
And my spirit has become feeble in me, My heart has become desolate within me.
5 Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
I have remembered days of old, I have meditated on all Your acts, I muse on the work of Your hand.
6 Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
I have spread forth my hands to You, My soul [is] as a weary land for You. (Selah)
7 Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
Hurry, answer me, O YHWH, My spirit has been consumed, Do not hide Your face from me, Or I have been compared with those going down [to] the pit.
8 Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
Cause me to hear Your kindness in the morning, For I have trusted in You, Cause me to know the way that I go, For I have lifted up my soul to You.
9 Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
Deliver me from my enemies, O YHWH, Near You I am covered.
10 Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
Teach me to do Your good pleasure, For You [are] my God—Your Spirit [is] good, Lead me into a land of uprightness.
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
You quicken me for Your Name’s sake, O YHWH, In Your righteousness, You bring out my soul from distress,
12 Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.
And in Your kindness cut off my enemies, And have destroyed all the adversaries of my soul, For I [am] Your servant!

< Zaburi 143 >