< Zaburi 142 >
1 Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
Intelligence de David, lorsqu’il était dans la caverne, prière. De ma voix vers le Seigneur j’ai crié: de ma voix au Seigneur j’ai adressé ma supplication;
2 Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
Je répands, en sa présence, ma prière; et ma tribulation, c’est devant lui-même que je l’expose.
3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
Pendant que mon esprit se retire de moi, et c’est vous qui avez connu mes sentiers.
4 Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
Je considérais à ma droite, et je regardais; et il n’y avait personne qui me connût.
5 Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
J’ai crié vers vous, Seigneur, j’ai dit: C’est vous qui êtes mon espérance, ma part dans la terre des vivants.
6 Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
Soyez attentif à ma supplication, parce que j’ai, été humilié à l’excès.
7 Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.
Retirez de la prison mon âme, pour qu’elle glorifie votre nom: des justes m’attendent, jusqu’à ce que vous me rendiez justice.