< Zaburi 142 >
1 Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
Hymne de David, lorsqu'il était dans la caverne. — Prière. Ma voix crie vers l'Éternel; Ma voix implore l'Éternel.
2 Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
Je répands ma plainte devant lui; J'expose ma détresse en sa présence.
3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
Quand je sens mon esprit défaillir en moi. Toi, tu connais le sentier où je marche. Dans le chemin où je m'avance. On m'a tendu un piège.
4 Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
Regarde à ma droite, et vois! Personne ne me reconnaît. Tout refuge me manque; Personne ne prend souci de moi.
5 Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
Je crie vers toi, ô Éternel, Et je dis: Tu es mon asile. Mon partage sur la terre des vivants.
6 Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
Sois attentif à mon cri; Car je suis extrêmement misérable. Délivre-moi de ceux qui me poursuivent; Car ils sont plus forts que moi.
7 Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.
Retire mon âme de sa prison, Afin que je puisse célébrer ton nom! Les justes viendront triompher avec moi De ce que tu m'auras comblé de tes bienfaits.