< Zaburi 142 >

1 Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
Instruction de David; lorsqu’il était dans la caverne. Prière. De ma voix, je crie à l’Éternel; de ma voix, je supplie l’Éternel.
2 Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
Je répands devant lui ma plainte, je déclare ma détresse devant lui.
3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
Quand mon esprit était accablé en moi, toi tu as connu mon sentier. Sur le chemin par lequel je marchais, ils m’ont caché un piège.
4 Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
Regarde à droite, et vois; il n’y a personne qui me reconnaisse; tout refuge est perdu pour moi; il n’y a personne qui s’enquière de mon âme.
5 Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
J’ai crié vers toi, Éternel! j’ai dit: Tu es mon refuge, ma part dans la terre des vivants.
6 Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
Sois attentif à mon cri, car je suis très misérable; délivre-moi de mes persécuteurs, car ils sont plus forts que moi.
7 Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.
Fais sortir mon âme de la prison, pour célébrer ton nom. Les justes m’environneront, parce que tu m’auras fait du bien.

< Zaburi 142 >