< Zaburi 142 >
1 Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
Yahweh, I cry out to you; I plead [with you to help me].
2 Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
I am bringing to you [all] my problems; I am telling you [all] my troubles/difficulties.
3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
When I am very discouraged, you know what I should do. Wherever I walk, [it is as though] my enemies have hidden traps for me [to fall into].
4 Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
I look around, but there is no one who pays attention to me, no one who will protect me, no one who cares about [what happens to] me.
5 Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
[So] Yahweh, I cry out to you [to help me]; you are the one who protects me; and you are all that I need while I am alive.
6 Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
Listen to me while I cry out to you [for help], because I am very distressed. Rescue/Save me from those who are pursuing me, because they are very strong, with the result that I cannot [escape from them].
7 Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.
Free/Rescue me from my troubles/difficulties [MET] in order that I may thank you. If you do that, when I am with godly/righteous [people], [I will praise you] for having been very good to me.