< Zaburi 142 >

1 Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
“A psalm of David; a prayer, when he was in the cave” I cry unto the LORD with my voice; With my voice to the LORD do I make my supplication.
2 Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
I pour out my complaint before him; I declare before him my distress.
3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
When my spirit is overwhelmed within me, Thou knowest my path! In the way which I walk, they have hid a snare for me.
4 Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
I look on my right hand, and behold, But no man knoweth me; Refuge faileth me; No one careth for me.
5 Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
I cry unto thee, O LORD! I say, Thou art my refuge, My portion in the land of the living.
6 Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
Attend to my cry, for I am brought very low; Deliver me from my persecutors, For they prevail against me!
7 Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.
Bring me out of prison, That I may praise thy name! The righteous shall gather around me, When thou shalt show me thy favor.

< Zaburi 142 >