< Zaburi 142 >

1 Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
Maschil of David, when he was in the cave; a Prayer. With my voice I cry unto the LORD; with my voice I make supplication unto the LORD.
2 Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
I pour out my complaint before Him, I declare before Him my trouble;
3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
When my spirit fainteth within me — Thou knowest my path — in the way wherein I walk have they hidden a snare for me.
4 Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
Look on my right hand, and see, for there is no man that knoweth me; I have no way to flee; no man careth for my soul.
5 Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
I have cried unto Thee, O LORD; I have said: 'Thou art my refuge, my portion in the land of the living.'
6 Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
Attend unto my cry; for I am brought very low; deliver me from my persecutors; for they are too strong for me.
7 Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.
Bring my soul out of prison, that I may give thanks unto Thy name; the righteous shall crown themselves because of me; for Thou wilt deal bountifully with me.

< Zaburi 142 >